Baadhi ya Wachezaji wa Ihefu FC Wakisherehekea Ushindi wao Dhidi ya Mashujaa FC |
Kocha wa
Timu ya Mashujaa Fc Mwana Mapigo na Mwendo Abdallah Mohamed Bares amesema
Michuano ya Kombe la Shirikisho (CRDB FEDERATION CUP) Ilikuwa ni ya Ziada kwa
kwani Malengo yao Makuu ni Kupambana Vilivyo Kujiweka Sawa kunako ligi Soka
Tanzania Bara.
Akizungumza
na Wanahabari Mkoani Singida Baada ya Timu yake Kuondoshwa kunako michuano ya
Kombe la Shirikisho kwa Mikwaji ya Penati (4-3) Dhidi ya Ihefu FC Katika uwanja
wa Liti Mkoani Singida Bares Amesema Timu hiyo sasa inahamishia Nguvu katika
Michezo iliyosalia katika Ligi Kuu Soka Tanzania Bara.
Kocha wa
Ihefu Fc Mecky Mexime wamewataka Mashabiki wa Kandanda Mkoani Singid Kuweka
Kando tofauti walizonazo na Kushikamana Pamoja ili Kuisapoti Timu hiyo ili
Ifanye Vizuri katika Hatua Inayofuata.
Nahodha wa
Ihefu FC Joash Onyango Achieng Ametawazwa kuwa Mchezaji Bora wa Mechi ya leo na
kuzawadiwa Kitita cha Shilingi Laki Tano kutoka wa Wadhamini wa Michauno hiyo
na Amewapongeza wachezaji wenzanke kwa Kiwango Bora walichokionyesha Katika
Mchezo huo.
Post a Comment